Tuesday, October 25, 2022

Tanesco -Saccos waungana na Tanesco Ltd katika ushirikiano bora


 

MKURUGENZI wa Rasilimali watu na Utawala wa Shirika la Umeme Tanzania ‘TANESCO’  Francis Sanguna amesema wamefanikiwa kusaini muswada wa kuwaunganisha  Tanesco Saccos na Tanesco Ltd  ili  kujenga mifumo imara na endelevu wa ukusanyaji akiba, hisa na amana.

Akizungumza na  jana wakati wa mkutano mkuu na  wanachama wa Chama cha Ushirika na Kukopa ‘Tanesco Saccos’  Sanguna alisema  duniani kote vyama vya ushirika na kukopa ni nguzo muhimu, na vimekuwa vinachangia ukuaji wa uchumi na  pato la taifa.

Alisema kati ya wafanyakazi 7000 wenye mikataba ya kudumua wafanyakazi 6000 ni wanavchama wa Ushirika huo, ambapo wanaendelea kuwashauri  na  wafanyakazi wapya   kujiunga.

"Vyama hivi vimekuwa na mchango mkubwa sana  ni nguzo ya uchumi wa nchi bodi ya Tanesco,  inatambua umuhimu huo na kutaka  uongozi wa Saccoss kutekeleza malengo yake  na kusimamia yale waliyojiwekea.

Wanachama waendelee kuchangia katika chama pamoja na kutumia mifuko ya Tehama ikiwemo huduma ya kiganjani kupitia simu," alisema

Mwenyekiti wa Chama cha Tanesco Saccos Somoe Nguhwe amesema pamoja na kutoa mikopo kwa wanachama, wamekuwa na utaratibu wa kujali  jamii kwa kutoa msaada.

  "Mkutano mkuu wa mwaka huu tunaangalia mapato na matumizi ili mwaka  2022 tujue tufanye nini, lakini pia  tunaendelea kuwa karibu na jamii kwa kwenda kutoa mashuka katika hospitali ya kansa  Ocean Road," alisema.


Katika mkutano  huo  wanachama waliweza kupatiwa tuzo na mgeni rasmi katika upande wa mwanachama bora katika uwekaji akiba, mwanachama bora upande wa mikopo na mwanachama bora  kwa upande  matumizi ya Tehama.

Naye mwanachama na mfanyakazi wa Tanesco Monica Masawe amesema chama hicho kimeweza kumsaidia kupata  mkopo wa elimu wakati anahitaji kujiendeleza, pia amesomesha watoto wake pamoja na kujipatia fedha za kuanzisha miradi midogo midogo ya ufugaji wa Kuku wa mayai.

mwisho

No comments:

Post a Comment

https://www.facebook.com/gomesamohamedi