MKURUGENZI wa Rasilimali watu na Utawala wa Shirika la Umeme Tanzania ‘TANESCO’ Francis Sanguna amesema wamefanikiwa kusaini muswada wa kuwaunganisha Tanesco Saccos na Tanesco Ltd ili kujenga mifumo imara na endelevu wa ukusanyaji akiba, hisa na amana.
Akizungumza na jana wakati wa mkutano mkuu na wanachama wa Chama cha Ushirika na Kukopa ‘Tanesco Saccos’ Sanguna alisema duniani kote vyama vya ushirika na kukopa ni nguzo muhimu, na vimekuwa vinachangia ukuaji wa uchumi na pato la taifa.
Alisema kati ya wafanyakazi 7000 wenye mikataba ya kudumua wafanyakazi 6000 ni wanavchama wa Ushirika huo, ambapo wanaendelea kuwashauri na wafanyakazi wapya kujiunga.
"Vyama hivi vimekuwa na mchango mkubwa sana ni nguzo ya uchumi wa nchi bodi ya Tanesco, inatambua umuhimu huo na kutaka uongozi wa Saccoss kutekeleza malengo yake na kusimamia yale waliyojiwekea.
Wanachama waendelee kuchangia katika chama pamoja na kutumia mifuko ya Tehama ikiwemo huduma ya kiganjani kupitia simu," alisema
Mwenyekiti wa Chama cha Tanesco Saccos Somoe Nguhwe amesema pamoja na kutoa mikopo kwa wanachama, wamekuwa na utaratibu wa kujali jamii kwa kutoa msaada.
"Mkutano mkuu wa mwaka huu tunaangalia mapato na matumizi ili mwaka 2022 tujue tufanye nini, lakini pia tunaendelea kuwa karibu na jamii kwa kwenda kutoa mashuka katika hospitali ya kansa Ocean Road," alisema.
Katika mkutano huo wanachama waliweza kupatiwa tuzo na mgeni rasmi katika upande wa mwanachama bora katika uwekaji akiba, mwanachama bora upande wa mikopo na mwanachama bora kwa upande matumizi ya Tehama.
Naye mwanachama na mfanyakazi wa Tanesco Monica Masawe amesema chama hicho kimeweza kumsaidia kupata mkopo wa elimu wakati anahitaji kujiendeleza, pia amesomesha watoto wake pamoja na kujipatia fedha za kuanzisha miradi midogo midogo ya ufugaji wa Kuku wa mayai.
mwisho

No comments:
Post a Comment
https://www.facebook.com/gomesamohamedi