BAADA ya
tasnia ya filamu ya Bongo Movies kuyumba mwigizaji wa filamu nchini Vicenti
Kigosi ‘Ray’ amesema bado hana imani na kuuza kazi yake katika mtandao ‘App’ kutokana na ubora.
Ray anasema tayari alishapitia ‘App’ mbalimbali za
Tanzania, lakini akagundua unaweza kupakua katika simu yako lakini ikashindwa
kuangalia video kwa utulivu sababu zinakwama sana.
Alisema
teknolojia yetu bado haina uwezo wa kumfanya mtu akatizama vizuri filamu kwenye
simu baada ya kupakua ‘app’ kama ilivyokuwa kwenye Cd.
Wasanii
ambao tayari wameshafungua ‘app’ zao na kuweka filamu zao huo ni Ahmed Salim
‘Gabo’ ambayo anamiliki ya Uhondo na Wema Sepetu ambayo hivi karibuni ameweka
filamu ya Heaven Sent.

No comments:
Post a Comment
https://www.facebook.com/gomesamohamedi