Tuesday, September 26, 2017

Shamsa Ford na Gabo hao



 Shamsa Ford  aanatarajia kuingiza sokoni filamu mpya ya  Sikujua akiwa na mwigizaji Salm Ahmed ‘Gabo’ huku akishikiria kwamba sasa hivi hawauzi  haki miliki.

Wawili hao waliweza kufanya vizuri katika filamu kali kama Bado Natafuta ambayo ilimtambulisha Gabo katika ulimwengo wa filamu hadi leo jina lake kuendelea kung'ang'ania juu.

Akizungumza filamu hiyo Shamsa  itakayoingia hivi karibuni hatouza haki yake isipokuwa kuna mtindo mpya wa kugawana mapato na msambazaji bila ya kununua haki.
Alisema kwa sasa hataki kuweka wazi ni njia gani ambayo kampuni hiyo mpya ya Kibalazani huitumia, lakini anaamini kwamba atapata manufaa na haki yake pia itabaki.
Anasema anaamini awamu hii ya pili ya uingiaji sokoni wa filamu utaweza kuwanufaisha wasanii.

No comments:

Post a Comment

https://www.facebook.com/gomesamohamedi