Na Mohamed
Mussa
KUTOKANA na
mfumo wa maisha ya sasa ulivyo kila mtu amekuwa akiangalia kile kinachotokeza
mbele yake na kukiona kama fulsa ya kujipatia kipato.
Hali hiyo
imelekea wahitaji huduma kutojua hasa
wapi sehemu husika ya kupata huduma ambayo wamekuwa wakiitaka kutokana na
matatizo yanayowaandama.
Lakini hali
imezidi kuwa mbaya zaidi baada ya baadhi ya watu kuchukulia ni fulsa hata vitu vya msingi ambavyo
havikuhitaji mzaha na ndipo husababisha matatizo kuongezeka zaidi badala ya kupungua.
Zamani
nilikuwa tukijua matatizo kama ya watumiaji wa madawa ya kulevya, yanahitaji
uangalifu wa hali ya juu sana sababu watu hao sio wanakuwa hatari tu kwa wale
wanaoishi nao ila huwa hatari hata kwa wao wenyewe.
Wapo ambao
walikuwa na malengo sahihi ya kutaka kuwasaidia kwa kufungua vituo stahiki
kwaajili ya kutoa huduma maarufu kama Soba, lakini kwa sasa mambo yamebadilika.
Leo vituo
vya Soba vimekuwa vingi na kufanya watu washindwe kujua hasa ni kipi kituo
sahihi kwaajili ya kusaidia waathirika.
Matukio kama
hayo yalishawakuta waanzilishi wa vituo vya watoto waishia katika mazingira
magumu, baada ya watu kuanzisha vituo kila mahali na kupelekea watu kutokuwa na
imani na vituo hivyo
Mwandishi wa
makala hii, alimfuata mwazilishi wa soba ya Pili Missanah Foundation na mwenyekiti
wa chama cha wamiliki Soba Tanzania ‘
Voice of Soba’ Pili Missahn ambapo
alifafanua zaidi jinsi wanavyoweza kukabiliana na matatizo hayo
wanawachukulia ni wezi,” alisema..
Anasema mara
nyingi jamii imekuwa ikipamba kuhakikisha
Soba zinaondolewa katika maeno yao, ingawa waathirika wanakuwa hawana madhara
kwakuwa hawatoki nje kwa takribani miezi tatu hadi sita.
Pili anasema
wamekuwa wakisaidia watu wengi sana
kupitia soba, lakini wanakabiliwa na hali ngumu ikiwepo kulipa kodi ya nyumba
kwakuwa hawawezi kuchukua nyumba lazima wakodi nyumba nzima.
Anasema hata
hivyo wamekuwa wakipata huduma mbalimbali kutoka Serikali na kwenye mashirikika
makubwa, hivyo mtu anapopata tatizo huwa
wanajiongeza zaidi kwaajili ya matibabu.
Pili
Missanah histori yake ya kuanzisha vituo hivyo ilianza mkoani Mwanza ambapo
alizaliwa akiwa na kabira la Msukuma,
ambapo alimaliza elimu yake ya sekondari
Mwanza secondary mwaka 2003.
Baada ya
hapo akajiunga na vituo vya kulelea watoto waishio katika mazingira
magumu, huku akiendelea na masomo yake
ya IT.
Mwaka 2006
akajitolea kupita mtaani kwaajili ya kuongea na waathirika wa madawa ya kulevya
na kuwapa ushauri, ingawa hakuwa na uwezo wa kusaidia chochote.
![]() |
| Mwandishi wa makala hii Mohamed Mussa Gomesa, akiwa na mwanamuziki Hawa maarufu kama Hawa Nitarejea au Hawa wa Diamond |
Ndipo
alipokuja Dar es salaam ambapo mwaka 2012 alipoamua kufungua kituo Kigamboni,
kwaajili ya kusaidia waathirika wa madawa ya kulevya.
Baada ya
kufungua kituo cha kwanza Kigamboni aliseza kupata msaada kutoka kwa Zacheria Hans Pope, ambapo tayari alikuwa na vijana zaidi ya 700
waliweza kujitokeza kupata huduma hizo.
Watu kutoka
makanisani na misikiti pia walianza kujitolea, hadi pale Hans Pope alipoamua
kuachana na kituo hicho kutokana na hali yake ya kimaisha.
Anasema hata
hivyo kituo kiliendelea kukua ba kuzaa
vituo vingine vinne wakati huo vituo
vitatu vikiwa Dar es Salaam pekee na kituo kimoja kikiwa Mwanza kipo kimoja.
Anasema Soba
za Dar es Salaam hadi sasa ina jumla ya
waathirika tofauti tofauti 93 wakati
kituo cha Mwanza kina waathirika tofauti tofauti 29.
Alisema
kituo hicho kina wafanyakazi wanaosimamia kituo wa kudumu ni watatu wengine 18 wanakuja na kuondoka
kwaajili ya kusaidia shughuli za kituoni.
“Kuna
kipindi tunahitaji baadhi ya watu kutusaidia, sababu hali inakuwa tofauti,”
alisema.
Anasema hadi
sasa kituo kimesaidia watu 1977 lakini watu zaidi ya 200 wamerudia tena katika
utumiaji, lakini wapo ambao wamearudia katika utumiaji wa madawa ya kulevya na
baadaye wakaona ni bora kurudi tena kituoni kwaajili ya kumalizia dawa.
“Wengine
wanakuwa wanaletwa na familia zao, hivyo wanaleta tabu na kusema kwamba akitoka
hapa anaenda kutumia tena,”alisema.
Anasema
kituo pia kimekuwa kikipokea watu wenye majina, wafanya kazi, watu maarufu na
wasanii ambao hawataki kutajwa majina yao wanakuja kituoni kwaajili ya kupata ushauri na elimu
juu ya kuachana na matumizi ya madawa ya kulevya ikiwemo pombe kali.
Pili anasema
kituoni hapo miongoni mwa huduma wanayoitoa ni
elimu ya mtu kujitambua na ni jinsi gani unaweza kuishi bila ya kutumia
kilevi chochote.
Anasema sio
ngumu kwa muathirika kuamua kuchana na madawa ya kulevya kama akiamua yeye
mwenyewe, kwakuwa atapata maumivu kwa
muda wa siku tatu baada ya hapo anakuwa sawa.
Anasema hawatumii dawa kwaajili ya kuwaachananisha na
madawa ya kulevya, isipokuwa wanawapa elimu,
ushauri na kuwafungia ndani ili wasiweze kutumia madawa hayo jambo ambalo
wanafanikiwa kuwasaidia pia.
Kuwaachisha
utumiaji wa madawa kunaendana na mpango maalumu wa unaojulikana kama ROSC ,
yaani uachaji wa kutumia madawa ya kulevya bila ya kutumia dawa.
“Huo mpango
unasaidia sana watu kuwafanya wajitambue, kwakuwa tunaenda kwa vipindi na huwa
hawatoki nje,” alisema.
Anasema kwa sasa wamekuwa wakipata msaada
kutoka Serikalini, kwenye mamlaka ya
kupambana na madawa ya kulevya na mashirikika mengine likiwemo shirika la umoja
wa mataifa.
Lakini
wanahitaji huduma zaidi kutokana na matatizo ambazo yanawakuta wakati mgonjwa
anapozindiwa.




No comments:
Post a Comment
https://www.facebook.com/gomesamohamedi