Huenda ikawa
ni hofu kutokana na mvua na ngurumo zinazoikabiri katika jiji la Mumbai, mwigizaji mkongwe wa
filamu Bollywood, Amitabh Bachchan ‘Big B au T 2552’ amesema chanzo cha mvua
hizo sababu mungu amekasirika.
Bachchan ambaye
anaushawishi mkubwa katika nchi ya India, aliandika kupitia akaunti yake ya
Twitter akiwataadharisha watu kutotoka nje kutokana na mvua hiyo kuto nyamaza
kunyesha.
Ameendelea kusisitiza
kwamba ngurumo za radi na miale mikali ya radi, ni salama zaidi kwa mtu kubaki
ndani kuliko kudharau jambo hilo.
Alitoa onyo
pia kwa Serikali yake kwamba hakuna mtu
ambaye anaweza kupambana na majanga asili kama Kimbunga Kizito, hata zile nchi
ambazo zinanguvu zaidi Duniani.

No comments:
Post a Comment
https://www.facebook.com/gomesamohamedi