Mwigizaji wa filamu na mwanamuziki Zuwena Mohamed
‘Shilole’ amesema ingawa amekaa kimya kwenye tasnia ya filamu lakini anajipanga
kurudi upya na kazi nzuri kwakuwa Bongo Movies kaona hawajitambui.
Shilole ambaye anaamini kwamba wasanii kuwa na kampeni nyingi ni sawa na kutojitambua, sababu hawajui wanataka nini.
Shilole ambaye anafanya vizuri na wimbo wake Kigoli, anamikakati ya kuwekeza fedha nyingi kwenye
mradi wake wa filamu kwakuwa hataki kurudia makosa yale yale wanayofanya
waigizaji wa filamu.
Aamewataka waigizaji
wenzake kutorudia stori, maeneo na kila kitu katika filamu zao ndio maana soko
la filamu za nje likachukua nafasi kwakuwa soko la ndani kama lilibaki wazi.

No comments:
Post a Comment
https://www.facebook.com/gomesamohamedi