MKALI wa
Bollywood na Brad Pitt ameamua kushirikiana na mkali wa Bollywood Shar Rukh Khan
kwaajili ya kuitangaza filamu mpya ya War Machine katika jiji la Mumbai.
Pitt ‘53’
alikutana na SRK kwaajili ya kuzungumzia masuala mbalimbali yakiwemo ya filamu,
pamoja na kufanya shughuli mbalimbaali zinazohusiana na filamu na kutengeneza
ukaribu wa kazi.
Katika
filamu hiyo ambayo inazungumzia tukio la kweli ambalo liliwahi kutokea,
imechezwa pia na waigizaji Ben Kingsley, Tilda Swinton, Anthony Michael Hall na
Topher Grace na kuongozwa na David Michod.
Alisema
filamu hiyo ambayo imechezwa katika nchi ya Afghanistan imetoka katika kitabu
cha The Operators: The Wild &
Terrifying kilichoandikwa na Michael Hastings.
Alisema yeye
aliigiza kama Kamanda wa jeshi la Marekani mwenye nyota nne akitumia jina
la general Glenn McMahon, aliyepambana
vita kati ya Marekani na Afghanistan.
Mvua hizo
zilipelekea baadhi ya shule na vyuo kufungwa kwa muda, huku baadhi ya maeneo
yakikubwa na mafuriko katika mji huo.

No comments:
Post a Comment
https://www.facebook.com/gomesamohamedi