Wakati wasanii wakiangaika kuwanadi wagombea wao, wasanii hao hao wameanza kutupiana maneno makali kiasi cha wengine kukasirika na kujibu tuhuma hizo. Mwigizaji wa filamu ya Chausiku, Shamsa Ford amejibu tuhuma za kwamba yeye anang'ang'ania UKAWA, kisa Ney wa Mitego.
Najua ninachokifanya na wala sijutii kwa ninachokifanya. Kila mtu ana maamuzi yake katika maisha yake .hakuna mtu wa kumpangia mtu kitu cha kukipenda au kukifanya. ...Nimeumizwa sana na haya maneno wanayoyaeneza watu mpaka kufikia kuniita mimi mjinga kwa mujibu wao eti nimekataa hela za CCM na kumfwata nay ukawa...Kitu kimoja naomba mtambue nyinyi mnaoniita mjinga kwamba nina misimamo yangu ya kimaisha na huwa siyumbishwi kwa kitu chochote. .Nimemuacha mtoto wangu nyumbani na familia kwasababu najua ninachokifanya. ....Sijamfwata mtu yeyote huku UKAWA zaidi ya kuamini kwamba nipo sehemu sahihi na nina imani na EDWARD LOWASSA kama wewe unavyomuamini Mgombea wako.KILA MTU AHESHIMU MAWAZO YA MWENZIE. #NAJITAMBUA # SUPERWOMAN

No comments:
Post a Comment
https://www.facebook.com/gomesamohamedi