Monday, July 28, 2014

Tego; nafanya tamasha Tabora sababu nakubalika



KIONGOZI  wa bendi ya Coast Modern taarab, Omari Tego amesema wanatarajia kufanya tamasha kubwa mkoani Tabora na mwanamuziki mwenzake  Hadija Kopa.


Tego alisema tamasha hilo wanatarajia kufanya kipindi hiki cha sikukuu  katika wilaya ya Urambo, baada ya hapo wanatarajia kuzunguka na wilaya nyingine.

Alisema bendi yake mara nyingi imekuwa ikikubalika eneo hilo, jambo ambalo anaamini watafanya vizuri kwakuwa na wapenzi wengi.

“Tunakubalika na ndio maana tunaarikwa kufanya tamasha eneo hilo, hivyo tunaahidi kutoa burudani ya nguvu,” alsema.

No comments:

Post a Comment

https://www.facebook.com/gomesamohamedi