Thursday, August 2, 2012

TWANGA, MASHUJAA, MAPACHA WA3, walichosema kwa Kalala Junior


Vuta nikuvute ya  wamiliki wa bendi juu ya  mwanamuziki Kalala Junior aliyekuwa bendi ya Mapacha Watatu yazidi kushika kasi. Kiongozi wa bendi ya  Mapacha Watatu , Jose Mara amesema kwamba  bendi hiyo, ingawa ameondoka mmoja kati yao lakini hatobadili jina kuitwa mapacha wawili, au kuchukuwa msanii yoyote mkubwa kwaaajili ya kuziba pengo hilo. Jose Mara amesema bendi hiyo jina la Mapacha Watatu lipo kama jina la usajili, na wala halibadiliki hata kama wakiondoka wote, hata hivyo amesema kuondoka kwa mwenzao mmoja wao bado wanaendelea kusonga, na hivi karibuni wametoa wimbo Ona Naonewa wakimshirikisha Ali Kiba. Pia walisisitiza na kusema hivi sasa watakuwa wakichukuwa wasanii wachanga  na kuwakuza wenyewe ambapo kwa sasa wanaye Jemsi Mavoko, Kambi Catherine, Adam wa Tabata na wengine wengi ambao wanafanya vizuri. Hata hivyo mwuisho walimalizia kwa kusema hawajui mwanamuziki huyo wapi anaelekea.

Wakati tetesi zikienea kwamba bendi ya Mashujaa maarufu kama muziki kazi, wakitarajia kumchukua mwanamuziki Kalala Junior kutoka katika bendi ya Mapacha Watatu, raisi wa bendi hiyo Chalz Baba amesema, Kalala Junior amewatolea mbavuni kujiunga na bendi hilo kutokana na matakwa yake kuhamia bendi ya Twanga Pepeta. Chalz alisema kwamba walishafikiana dau, lakini mwanamuziki huyo alikataa katakata, kwa madai kwamba hayupo sawa kukaa kwenye bendi hiyo ambayo pia yupo rafiki yake mpendwa ambaye ni Chalz na ndiye alikuwa akiongea naye juu ya kuhamia bendi hiyo.
Kasi zote za mwanamuziki Kalala Junior zinasemekana kuishia Twanga Pepeta na kutambulishwa siku ya jumamosi ya wiki hii katika viwanja vyao vya kila siku, lakini kiongozi na msemaji wa bendi hiyo Hassan Rehani amesema bendi yake haina mkataba wowote na wala haijaongea chochote na mwanamuziki huyo juu ya kuhamia bendi yake.

No comments:

Post a Comment

https://www.facebook.com/gomesamohamedi