Saturday, August 4, 2012

Linah aeleza juu ya uhusiano wake mpya

Mwanadada anayevuma na nyimbo kali kama vile  Fitina na aliyekuwa mpenzi wa mwanamuziki mwenzake kutoka Jumba hilo la vipaji Tanzania 'T.H.T' Amini Mwinyimkuu 'Amini',  amefunguka juu ya uhusiano wake mpya  na mpenzi wake ambaye raia wa State  Marekani. Linah alifunguka kwa kusema mpenzi wake huyo kwamba hapendi  ajihusishe na muziki,  jambo ambalo Linah alikataliana nalo kwa kumwambia  muziki upo ndani ya damu yake. Linah aliongeza kwa kusema mpezi wake huyo kwa sasa anatarajia kushuka Nchini Tz muda wowote kwaajili ya kumvisha pete ya uchumba kabla ya kuondoka kurudi tena State.  Linah alidai kwamba baaada ya pete ya uchumba matarajio  makubwa yatakuwa kwenye ndoa. 


Linah alizidi kuchonga kwamba hata kama akiolewa lakini hayupo tayari kwenda kuishi nchini Marekani, kwakuwa anaipenda Tanzania yake, na yupo radhi kwenda kila baada ya muda fulani nchini huko kwaajili ya kumfuata mmewe ambaye mfanya kazi na kisha kurudi. Pia lina alidai kwamba ingawa alikuwa nchini Marekani takribani  miezi mitatu, katika Tour ya Tumaini lakini hakuweza kumtafuta mpenzi wake huyo na wala hakuonana naye mpaka anarud kutokana na umbali wa miji aliofika yeye wa Dc Washngton na anapoishi mpenzi wake Atranta. Mwisho alimalizia kwa kusema hivi sasa anapoongea tayari gari lake limeshafika, anasuburi kumalizia harakati fupi aliingizeKitaaa


Linah na Amini kwenye pozi, huku wakijiandaa kuachia wimbo utakao kwenda kwa jina la Linah na Amini

No comments:

Post a Comment

https://www.facebook.com/gomesamohamedi