Tuesday, July 3, 2012

Mwandishi wa filamu ya Wema Sepetu afunguka

Mwandishi wa filamu ya Super Star ya Wema Sepetu,  Suma Lee  amesema uhaba wa fedha ziliichelewesha filamu hiyo kutoka ingawa aliiandika tangu mwaka 2010 na kuipitisha kwa wasanii mbalimbali ambao aliamini mwenye uwezo angeweza kuichukuwa na kuigiza lakini hatmaye ilishindikana kutokana na ghalama zilizohitajika katika filamu hiyo.
Suma Lee ambaye ni msanii wa muziki wa kizazi kipya alisema,  aliandika filamu tano, na kuanzi kuzipitisha kwa hao akiwemo mwigizaji  Swebe na Nteze lakini zilishindwa kufanyiwa kazi kutokana na ghalama ambazo msanii ilipaswa kuzitimiza katika uigizaji mzima wa filamu hiyo.
Aidha alidai kwamba  mtu wa kwanza kumpa tumaini kwamba angeichukuwa ni Jack Wolper, lakini ilishindikanika baadaye kutokana na kutingwa na kazi nyingi.
“Jack ndiye aliyempigia simu Wema na kumwambia kuhusu filamu hiyi,  na ndipo akanitafuta kwaajili ya kuiangalia na kuifanyia kazi” alisema.
Alisema wakati Wema Sepetu akiigiza filamu yake akiwa na Jacob Stephan ,lakini ikabidi aisimameshe filamu hiyo na kuiangalia filamu ya Super Star, ambapo aliipenda .
Filamu hiyo ilianza kubadilishwa vipengele vichache, kwakuwa ilikuwa ni stori ya kiume na sasa ilibadilishwa mpaka kuwa ya kike.
Ndipo stori nzima ilianza kufanana na maisha harisi ya Wema mwenyewe, hali ambayo ilisababisha hata Suma Lee kuchukua kiasi kidogo cha fedha ili filamu hiyo ikamilike.


No comments:

Post a Comment

https://www.facebook.com/gomesamohamedi