Tuesday, July 3, 2012

Ditto awaza soko la nje

NYOTA  wa muziki wa kizazi kipya kutoka nyumba ya Vipaji Tanzania ‘THT’ Lameki Ditto ‘Dito’, amesema anatarajia kuachia wimbo wake mpya wa Niamini, baada ya kumaliza safari zake za nje ya nchi.

Ditto alisema kimya chake kikubwa tangu alipotoa wimbo wa Tushukuru kwa wote,  ni kutokana na safari kuwa nyingi za  kimuziki iliyochukua muda mrefu katika nchi ya Kenya na Uganda.

Alisema akishatoa wimbo wake huo ataanza mikakati yake, aliyoipanga kwaajili ya kufanya kazi na wasanii wan je akianzia na Zambia.

“Nimefungua mtandao wangu kwaajili ya kusambaza kazi zangu nje, kwakuwa lengo langu sasa ni kufanya kazi na wasanii wan je|” alisema.
Aliongeza kwa kusema pia kwa sasa amefungua mtandao wake, ambao utakuwa maalumu kwaajili ya kazi zake za kimuziki, na kile ambacho yeye anaamua kukueleza kwa wananchi basi atatumia mtandao huo.



No comments:

Post a Comment

https://www.facebook.com/gomesamohamedi