Tuesday, July 10, 2012

Choki aigeukia Filamu

Nyota wa muziki wa Dansi nchini pia ni mmiliki wa Bendi ya  Extra Bongo ‘Wazee wa Kizigo’ Alichoki  kwa sasa anasema malengo yake ni kuanzisha kampuni itakayoshughulikia masuala ya filamu, baada ya kuona muziki ameushika vizuri.  Choki ambaye kwa mara ya kwanza filamu hiyo ilipaswa kuigizwa  Juni 30,  Mombasa nchini Kenya,  lakini kutokana na  kutingwa kwa kazi mbili moja ikiwa kufungua Bar yake na yapili ni uigizaji wa filamu hiyo ambayo bado hajaanza kuitangaza rasmi.  Anasema Ingawa kwa sasa analisaidia kundi la Choki Arts Group, ambayo tayari imeshakamilisha filamu  ya kwanza ambayo amewashirikisha Patcho Mwamba, Dude na Rehema Fabian na wakali wengine.  Ila pia anamikakati ya  kuanzisha kampuni hiyo ya filamu ambayo pia atahita kwa jina hilohilola Choki,  akiwa na lengo la kuinua vipaji vipya.   Aidha alidai kwamba kampuni hiyo  pia itakuwa ikishirikiana na wasanii wakongwe kwenye tasnia ya filamu ili kuweza kusaidia hao wasanii wachanga.   “Nataka niwe na kampuni ambayo imekamilika vifaa, na ofisi kabisa kwamba kilakitu kitakuwepo hapo” alisema

No comments:

Post a Comment

https://www.facebook.com/gomesamohamedi