Tuesday, July 10, 2012

Mkwabi wa 69 Record aumizwa na ndoto zake

Kwa sasa msanii kutoka Nyumba ya vipaji Tanzania, Juma Mkwabi anazidi kupata umaarufu mkubwa kutokana na ushiriki wake ndani ya tamthiria ya 69 Record inayorushwa na Clouds Tv.
Mkwabi anasema kwa sasa hatarajii na wala hafikirii kurudi tena kwenye muziki wa Hip Hop, inagaw mwanzo alikuwepo huko na kama akirudi basi atakuwa akiimba kama starehe. Aidha alisema kwamba muziki wa Hip Hop,  aliuanza tangu mwaka  1999,  lakini hakuweza kufanikiwa wala kuwa na umaarufu kama alionao sasa.

Aidha alidai kwamba mjomba wake, ambaye pia ni mwigizaji mwenzake Mpambala alianza kumfanyia mipango na kujiingiza sanaa ambapo alijikuta akifanya vizuri kuliko hata kwenye muziki. Alisema kwa sasa amefanya kazi na waingereza inayoitwa CPU, akiwa na lengo latuzo za kimataifa, pia amefanya kazi na mjomba wake Mobb ya Ant Virus akiwa kama Star, nab ado anashirikishwa kama mwonekanano katika wimbo na sio mwimbaji.

Lengo lake kubwa ni kufanya kazi za kimataifa na kupata tuzo kubwakubwa, pia alisema kwamba THT ndiyo nyumbani. hata hivyo amesema kwa sasa anahitaji sana kufanikisha malengo yake na sio umaarufu, na ndiyo maana anajaribu kukwepa umaarufu kabwa ya kupata fedha na mafanikio yale anayoyahitaji, sababu anaweza kueleza ndoto zake lakini zikashindikana kutokana na umaarufu



No comments:

Post a Comment

https://www.facebook.com/gomesamohamedi