Friday, June 1, 2012

Lady Jay dee arudi kutoka Masomoni

Mwanamuziki Lady Jay Dee amewasili  leo saa 7:45 mchana katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere  Jijini Dar es salaam akitoka  Afrika Kusini katika jiji la Cape Town, alipokuwa akisoma masomo ya muziki ya jukwaani 'Live Band'.   Jay Dee alisema hali ya hewa ya Cape Town  ni ya baridi sana  na nyuzi joto ilifikia  14 C, hali iliyosababisha apate shida kutokana na baridi kuwa kali sana. Mwanamuziki huyo anatajia kupanda jukwaani pamoja na bendi yake ya machozi leo, ili kukumbushia enzi zake kutokana na kuwa  nje ya nchi kwa muda mrefu. Jay dee anatarajia kurudi masomoni  Januari mwakani.
Jide akiwa na mumewe Gadner na mfanyakazi wa ndege.
Kaptain Gadner akimsaidia jide Begi.


Kaptaiiin G. Habash  na Jide wakiingia kwenye gari la Machozi Bendi kwaajili ya kwenda  Kinondoni, wanapoishi.

No comments:

Post a Comment

https://www.facebook.com/gomesamohamedi