NYOTA wa
muziki wa kizazi kipya na mwanadada
aliyediriki kukaa kwenye tasnia ya muziki wa kizazi kipya, kuliko wakinadada
wote Judith Wambura maarufu kama Binti Machozi, Komandoo, Jide, Lady Jay Dee na
majina mengi zaidi amefunguka baada ya kutua nchini kama wiki hivi kwa kusema muziki wa Tanzania bado umekuwa tatizo katika la kutochezwa jingo zetu katika Media hizo, ikiwemo Afrika Kusini, ambapo alikuwepo kwenye masomo
katika jiji la Cape Town.
Jide alisema ingawa Media zetu zimekuwa zikiwaunga mkono kwa
kupiga nyimbo zao, kwa wingi lakini nchi hizo zimekuwa hazipi Airtime, nyimbo
zetu.
Alisema
wakati yupo masomoni katika jiji hilo, hakuwahi kusikia nyimbo za Kibongo katika stesheni yoyote, zaidi ya wenyewe kwa wenyewe kusikilizishana,
kwa kusambaziana Cd. Hata hivyo ameshauri wadau na wasanii wa muziki kuthamini
cha kwetu, kwani kitapelekea kufika mbali na watu, kuvithamni baada ya sisi
kuthamini cha kwetu.
Jay dee
anatarajia kurudi tena masomoni, Januari mwakani ambapo ataenda kumalizia
masomo ya muziki wa jukwaani ‘Music Arts Perfomance’ maarufu kama Live band.
|
No comments:
Post a Comment
https://www.facebook.com/gomesamohamedi