Monday, June 11, 2012

Mwanza kutafuta msanii atakaye iwakishia Bongo

Kundi la wasanii wa muziki wa kizazi kipya wanatarajia kufanya Tamasha mkoani Mwanza kwaajili ya kumtafuta msanii chipukizi ambaye atapata nafasi ya kuja kuingia studio jijini  Dar es salaam.
Kundi la wasanii wa muziki wa kizazi kipya wanatarajia kufanya bonge la tamsha kwaajili ya kumtafuta mkali wa Mwanza, ambaye watakuja naye Dar es salaam kwaajili ya kufanya naye kazi zake za muziki akiwa Dar es salaa.

Wanamuziki hao ambao wakiongozwa na Saidi Fella, alisema tamasha  litafanyika mwezi  ujao katika viwanja tofauti tofauti ikiwemo tarehe 6 julai, Villa Park,7  Geita ukumbi wa Ambassador,  wakati tarehe 8 watamalizia katika kiwanja cha CCM Kilumba.  Miongoni mwa wasanii ambao watakuwemo kwenye tamasha hilo ni Ommy Dimpozi, Hamisi Mwijuma ‘Mwana Fa’,  Amani Temba ‘Mh Temba’, Hija Cheka ‘Bibi Cheka’ Ferooz ambaye ataenda kuitambulisha Kibodaboda, H. Number ‘Kasoro wewe’ na mzee wa Kitorodo ‘Nurudini’ . Wasanii wote wa Tmk pamoja na wasanii wa Mwanza. “Ni tamasha ambalo tutachagua msanii bora ambaye tutamsaidia,ili aweze kufika malengo yake  ya kimuziki” alisema Fella.  Msanii atakayefanikiwa kufanya vizuri atahamishiwa jijini Dar es salaam kwaajili ya kazi zake za kimuziki chini ya Mkubwa Fella.

No comments:

Post a Comment

https://www.facebook.com/gomesamohamedi