Wednesday, June 27, 2012

Dotnata aja na Homa Jiji

Mwigizaji wa filamu na mwanamuziki wa muziki wa dansi, Husna Poshi ‘Dotnata’ amesema kundi lake la  Homa Jiji sanaa Group  limeshaanza kukomaa kwaajili ya tamthiria itakayoanza mwezi ujao.
Aliimbia safu hii kwamba tamthiria hiyo, anatarajia itatoka mwezi ujao ingawa bado hajajua atatoa kwenye  stesheni ya Tv au atatumia utoaji wa Cd kama Season.
Pia lisema kwamba hatokuwa na kinyongo kwa msanii yoyote kutoka katika kundi hilo, endapo atacheza filamu nyingine yoyote kwakuwa lengo lake ni kuinua vipaji vipya.  “Sina Kinyongo kwa yeyote atakaye fanikiwa kwenye kundi langu na kuamua kufanya kazi nje, nitakuwa huru sana” alisema.

No comments:

Post a Comment

https://www.facebook.com/gomesamohamedi