Sunday, May 13, 2012

Ngwear aeleza malengo ya kampuni yao ya Radar Ent

MSANII  Robert Mangwer ‘Ngwear’ amesema kuungana kwa kundi la Radar Entertaiment ni kufufua vipaji vya wasanii wapya ambao wamekuwa na kipaji lakini wamwekosa msaada wa kurekodi. Akizungumza na mwandishi wa safuu hii alisema kampuni hiyo inaundwa na wasanii, Roomy Jonson ‘Rj’ Kharid Mohamed ‘TID’  Country Boy  na Bobuu wa Kitaa ambao.  Alisema  kampuni hiyo ya muziki  tayari imeshandaa  kipindi cha Tv cha  Talk Show, ambacho kitakuwa kikizungumzia mambo mbalimbali ya wasanii pamoja na matukio ya show mbalimbali.
“Lengo letu kwa sasa ni kuitambulisha kampuni watu waijue, kisha ndipo tuanze mikakati ya kuinua vipaji vipya ambavyo vimekosa msaada katika muziki” alisema.
Kundi la Radar tayari limeshakamilisha albamu moja, na hivi sasa wanatarajia kuachia wimbo Tunakiki alioshiriki Tid na Ngwea.