Sunday, May 13, 2012

Filamu yavamiwa na warembo

Mwigizaji maarufu wa filamu nchini Richie Rich, hivi sasa amejipanga katika ujio wa filamu yake mpya ya Uyoga,ambayo amekutanisha warembo ambao huenda hujawahi kuwaona katika filamu yoyote. Nifilamu ambayo kwangu mimi natamani sana sikumoja nije kuiona, maana wamejaa wasanii ambao wengi ni wale wanaochipukia na kutokea sehemu mbali mbali kama Miss Kinondoni mwaka 2011 Stera na Miss Arusha mwaka 2011 Aisha. Pia nimekutana na watu ambao huwa napenda sana kuona kazi zao kama Seleman Barafu, Hatman, Recho na Libert.
Hapa unaweza ukadhani wapo kwenye uigizaji lakini aliyevaa shati jeusi yeye ndiyo Cameraman, ila wote walipitiwa kwa mawazo juu ya kile ambacho walikuwa wakifikiria kukifanya.
Kulia ni Mr Kupa na kushoto wake ni Sudi wakiwa na Stera wa miss Kinondoni, vijana hawa wawili ni hatari katika kuchekesha, yaani ukikaa nao ujiandae sana, na kama hukucheka basi hutaweza kucheka tena.
Hata wakibishana, hebu waangalie jinsi walivyotulia.
Picha ambayo warembo,ambao wakiwa kwenye chumba chao wakijipaka Make up kwaajili ya kuingia mzigoni.
Miss Kinondoni Stera na Miss Arusha Aisha mambo yalikuwa hivi.
Seleman Barafu, akiwa kwenye pozi akisubiri kuingia kwenye shooting
 Hatmam
Libert
Libert

Hebu angalia