| Mamiss Tanzania mwaka 2006 - 2007 wamekuwa wakiliteka jiji huenda kuliko msimu wowote wa Mamiss ambao umewahi kupita katika nchi hii. Huenda haitatokea tena mamiss ambao wenye mbwembwe, ushindani, majigambo, ubabe, na wenye vituko kama msimu wa 2006 kwenda 2007. Kila mmoja alipart kwa wakati wake kama Movie, ili kuonyesha kwamba yeye anaweza, hawa ndiyo wamekuwa vinara kwenye magazeti na kufanya jiji lichangamke kwa mambo yao, tofauti na nchi za wenzetu ambapo wanamuziki huwa na vituko zaidi kama ilivyo kwa Beyonce, Nick Minaj, J.L, Witney wiston, Rihanna na wengine ambao wanaleta raha na karaha kwenye miji yao. Hapa kwetu kama ilivyo kwa cheo chake, tunaye Miss wa wa kwanza Tanzania mwaka 2006 - 2007 Wema Sepetu bingwa wa Skendo, pia wakafuata wengine... ambao wote walikutana jukwaa moja mwaka mmoja. |