Sunday, May 20, 2012

BASATA wadai Cyrill si Mtanzania

Uzinduzi wa Documentary ya mwanamuziki wa Bongo Fleva Cyril umeanza kuingia nuksi baada ya Baraza la Sanaa Tanzania ‘BASATA’ kumtumia barua ya kuomba atoe maelezo kwaana kwamba msanii huyo sio mtanzania ila ni Mkenya.
Jambo hilo limemshangaza sana msanii huyo kwa madai kwamba yeye ni Mtanzania harisi, na wala hayo ambayo anaamibiwa yeye hayajui.
“ eti wanasema NIMETENGENEZA skendo...huu ndio uthibitisho namba 1,namba 2 ni mazungumzo ya simu baina yangu na bosi wa BASATA leo mkuu Bwana LUHALA yalio rekodiwa” alisema msanii huyo baada ya watu kuhisi huenda kufanya hivyoni kujipigia chapuo ili afanye vizuri kwenye uzinduzi huo.
Lakini Cyril alisema ingawa alitumiwa barua hiyo, lakini kwake bado hajasitisha suala la uzinduzi wa Documentary hiyo pale Maisha Klabu siku ya leo jumapili, kwakuwa yeye ni Mtanzania harisi.
Barua toka BASATA