| Uzinduzi wa filamu ya TOBA katika ukumbi wa Safari Hall uliopo Bwawani katika mji wa Zanzibar umeonyesha wazi jinsi watu wa Zanzibar wanavyomkubali msanii Issa Mussa 'Cloud 112' , na kumjengea tumaini msanii huyo katika mji aliozaliwa. Uzinduzi huo ambao mgeni rasmi ni Makamu wa raisi wa kwanza Zanzibar Maalim Sefu sharifu Hamadi (wa katikakati), pia uliudhuliwa na viongozi mbalimbali wa serikali ya Mapinduzi Zanzibar akiwemo, Spika wa baraza la wawakilishi Zanzibar Mh Pandu Ameir Kificho(Kushoto aliyevaa kanzu nyeupe), waziri wa Utamaduni na michezo Zanzibar Said Ali Mbarouk, mkuu wa mkoa mjini magharibi na wengine wengi. Wananchi wa mjini Zanzibar waliudhulia kwa wingi kiasi cha kupelekea kuisha hadi tiketi za ziada, hali ambayo ilisababisha ukumbi kujaa, na wengine kubaki nje kwa kukosa tiketi sababu ndani kulijaa sana. Pia katika uzinduzi huo Cd za filamu ya TOBA , ziliuzwa kwa mnada huku Waziri wa utamaduni na michezo pamoja na mama Loraa walinunua parti 1 & 2 kwa shilingi laki 2. Cd zingine ziliuzwa kwa laki moja, elfu 50, elfu 20 na zingine zikauzwa kwa shiling 10000na 5000,ambapo zikaisha zote. Maalim Sefu alisema tukio hilo litabaki katika histori kwakuwa hakuwahi kuona ukumbi wa Safari Hall ukijaa kama ulivyo jaa, ila alimshauri Cloud 112 na wasanii wengine kwamba, watakapohitaji kufanya tukio lingine kama hilo, basi waombenafasi ya uwanja wa kutosha. |