Sunday, May 27, 2012

Dogo asalay aja na kitu kipya na kuwapotezea majimama

Nyota wa muziki wa kizazi kipya Aslay Sadiq 'Dogo Aslay' ambaye alitamba na wimbo wa Naenda kusema na Nawe nawe, anatarajia kuachia ngoma yake ya tatu inayokwenda kwa jina la Umbea umbea. Aslay alisema wimbo huo ambao ameufanya chini studio ya Poteza Record kwa Suresh 'Mr India' amemshirikisha Saidi Juma 'Chege' na ni miongoni mwa wimbo ambao anaupenda sana. Alisema wimbo huo ataanza kuutoa kwa njia ya video ambayo ameitengeneza Adam Juma wa Next Level.

Aslay pia alidokeza alisema ingawa kwa sasa anasumbuliwa na majimama mijitu mizima, lakini amekuwa nao mbali sana kwakuwa hivi sasa lengo lake likiwa katika kusoma na kuona fani ya muziki inaendaje.

Dogo Aslay akiwa na mdogo wake Dogo Muu ambaye anakuja na filamu ya Shahidi.

No comments:

Post a Comment

https://www.facebook.com/gomesamohamedi