Sunday, April 29, 2012

Pacha wa Cloud awasili kuangalia afya ya kaka yake

mwigizaji maarufu wa filamu nchini Issa Mussa 'Cloud 112' hivi karibuni aliugua ghafla na kupelekea kulazwa katika hospitali iliyokuwepo kariakoo ya Al Ijumaa. Lakini mwigizaji huyoamesema kwa sasa hali yake inaendelea vizuri na tayari amesharuhusiwa na amerudi nyumbani  na kuendelea na kazi zake. lakini hali hiyo ilipelekea mdogo wake ambaye ni pacha wake anayeishi mjini Zanzibar kuwasili haraka kwaajili yakumwangalia pacha wake
Khalfan pacha wa Cloud112 akiwa amemshika mtoto wa Cloud Nabil 'Prince, Cloud Junior'. Khalfan amesema yeye ameshika sana upande wa dini, na hawezi kushirikiana na kaka yake katika masuala ya filamu. hata hivyo anamuombea sana duwa siku moja aachane na kuigiza na kufanya kazi zingine kwaajili yakumtukuza Mungu
Khalfan Cloud 112 na Cloud jr