Sunday, April 29, 2012

Five Star kuzindua albamu mpya

BENDI ya  ya Five Star Modern Taarab inatarajia kuingia kambini katika kuandaa albamu ya pili  tangu ilipopata ajali na kupoteza wanamuziki wake.   Kiongozi wa bendi hiyo Ally Juma ‘Ally Jay’ , alisema albamu hiyo itakuwa ya pili baada ya ile ya Riziki mwanzo wa Chuki, ambayo itabeba nyimbo tano hadi sita.
Alizitaja baadhi ya nyimbo ambazo zitakuwepo  ni kusema mtasema vibaya kutukanana, Silipizi kwa ubaya,  na nyingine ambazo tayari na zingine zinatengenezwa studio.  “Mashabiki wa Five Stars naomba waendelee kuifuatilia bendi yao kama zamani, ili waweze kujua nini tunatajka kukifanya” alisema
Bendi ya Five Stars Modern taarabu ilipoteza wasanii wake 13 katika ajali iliyotokea Morogoro mwaka jana March na kumpoteza mwimbaji wake mahaili Issa Kijoti.