| Minong'ono ilianza tu, pindi ilipowekwa picha hii katika maombolezo ya kifo cha nguli wa filamu nchini R.I.P Steven Kanumba, kutokana na alama hiyo kuhusishwa moja kwa moja na alama za mashetani maarufu kama Freemasonry chini ya kiongozi wao Lucefer. Watu walijadilikwamba hakukuwa na picha nyingine nzuri zaidi ya hii, au hiyondiyo waliipenda sana. Hata hivyo baadhi ya wasanii na wadau wengine walisema hiyo ni picha kama picha nyingine,ingawa ilikuwa na maana zaidi na huenda yule aliyevaa asijue maana yake. Ndipolikaja neno kwamba, kama ndiyo hivyo basi wasanii wengi watakuwa wakitumiwa na mashetani, bila ya wao kujijua na hatmaye vifo vyao vikawa kamandoto..... |