Mwanamuziki Badibakule kutoka nyanda za kusikini na kuibuka kwa mara ya kwanza katika bendi ya African
Revorution ‘Wanatamatama’ na kutamba na
nyimbokama ‘Nipishe’ chini Mwijuma Muumini hivi sasa ameungana na kiongozi wake huyo wa zamani
katika bendi ya bendi ya African Stars ‘Twana Pepeta’. Badibakule
anasema kwake ni kama sehemu ya kurudisha jina lake ambalolimepotea ingawa siku zote bado yupo
kwenye bendi. Alisema
kufanya kazi na bendi hiyo, si jambo geni kwake kwakuwa hata African
Revolution, iliyomtambulisha kwenye muziki ilikuwa chini ya Asha Baraka na sasa
hivi yupo tena chini ya huyo huyo. Mwanamuziki
huyo kwa miaka kadhaa alikuwa katika bendi ya
T.OT Plus na baadaye kujiunga na
Lavent Music ya Morogoro. Katika bendi
yake ya Morogoro alikaa kwa muda wa miezi minne, na jumaanne ya April 18 ndipo
akajiunga rasmi na bendi ya Twanga. Anasema
alipojiunga na bendi hiyo alifanya tamasha lake la kwanza, katika viwanja vya
Club Bilicanas siku ya juma tano, kwasasa anatarajia kufanya tena tamasha katika viwanja vya Leaders Club juma
mosi. Hata hivyo
alisema kwamba hajasaini mkataba wowote, ila wamekubaliana kwa njia ya mdomo,
huku akiendelea na kazi.
Pia kiongozi
wa bendi hiyo Hassan Rehani, alisema kwamba mikataba ya wachezaji mpira ndiyo
mara nyingi imekuwa ikiheshimiwa, lakini ya wanamuziki imekuwa tofauti sana. Kiasi cha kutoitilia
mkazo kwakuwa hata wanapowasainisha, basi wanamuziki hao wanapoamua wanaondoka
na ndiyo maana wanatumia makabaliano ya mdomo.
|