Thursday, March 8, 2012

Vichwa vilivyotoka Twanga na kisha kuigeukia Twanga

Hawa ndiyo wasanii wakali wanne ambao kwa sasa wamekuwa waongozaji wa kubwa katika bendi ya Mashujaa Bendi na wote hawa asili yao wametokea kwenye bendi ya Twanga Pepeta na sasa wamekutana tena. Aliyevaa mawani ni kiongozi wa kundi hilo ambaye yeye ndiye anayechagua ni nani anamtaka kwenye bendi yake anaitwa Jadol FFU amabaye kabla ya kuwepo hapoa alitokea Twanga, anayefuata na Chaz Baba ambaye alitikisa sana katika bendi ya Twanga Pepeta na hatmaye na katua hapo na aliyevaa kaperompiga gitaa la Solo huku akiwa kiraka wa kila sehemu Ali Akida nadhani kwa wale wapenzi wa Twanga Pepe na muziki wa Dansi wanamjua sana, na pembeni yaoni Lilian Internet naye kwa sasa ingizo jipya la Mashujaa akitokea Twanga pepeta mambo ndiyo hivyo.
Ali Akida akiwa na wapiga gitaa wapya katika bendi mpya ya Mashujaa, lakini hata hivyo anasema bado hajapata mkataba, kwani akishakamilisha huomkataba lazima akaonane na Asha Baraka wa Twanga Pepeta na kukabidhi barua ya kuondoka kwake.
Chini ni Lilian Internet yeye alichukuliwa kwa dau la Milioni tanokwa kuhamishwa tu,kisha akapangiwa nyumbakodi laki mbili, kisha mshahara juu,kwa kazi ya unenguaji katika bendi hiyo mpya na hapa tayari akianza kujinoa kwaajili ya kuanza kazi
 Ch