Tuesday, October 4, 2022

Mama Ongea na Mwanao waanzisha kampeni ya kuchangia viatu wavuta viatu 450 na Sh Mil 65.9

TAASISI ya wasanii ya Mama Ongea na Mwanaye chini ya mwenyekiti Steve Mengele 'Steve Nyerere' wamekusanya zaidi ya jozi 450 za viatu na sh milioni 65.9 katika uzinduzi wa kampeni ya Samia Nivishe Kiatu.


 Akiongea katika uzinduzi huo uliofanyika  jijini Dar es Salaam, Steve alisema kampeni hiyo kwaajili ya kuwavesha viatu wanaufunzi wa shule za msingi hapa nchini. 


 Alisema katika kampeni hiyo wamefanikiwa kukusanya zaidi ya jozi 450 za viatu kutoka katika taasisi mbalimbali ambapo Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania ( TPA) waliochangia Sh Milioni 65.9. " Tunatarajia kuzunguka nchi nzima kuhakikisha tunawavisha watoto viatu sisi wenyewe. 


 Katika kampeni hii tutashirikiana na wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya pamoja na shule za msingi" alisema Mwakilishi wa mkurugenzi mkuu wa TPA, Beatrice Jairo alisema wameunga mkono taasisi hiyo kwakuwa wamekuwa na kawaida ya kutenga fungu kidogo kwaajili ya kuwarudishia wananchi kwa kile walichokipata Alisema tayari kila kitu kimekamilika ambapo wanatarajia kuanza muda wowote ila wataanza na Zanzibar.

No comments:

Post a Comment

https://www.facebook.com/gomesamohamedi