MKURUGENZI wa
bendi ya Mashauzi Classic, Isha Ramadhani ‘Isha Mashauzi’, amesema anatarajia
kuzindua albamu mbili kwa pamoja kama zawadi kwa mashabiki zake.
Isha alisema
kwa mwaka huu amejipanga kufanya kazi nyingi zaidi, ndiyo maana ameamua kutoa albamu hizo mbili,
Wasafi wa Mavazi wachafu wa Nafsi na Asiyekujua Akuthamini.
Alisema
wasubiri mashabiki wake kwani kuna vitu vipya ndani ya albamu hiyo, ambayo
kamwe hakuvifanya mwaka jana.
“Mashabiki
wasubiri kazi nzuri zinakuja, nitajitahidi kufanya kazi ambazo wamekuwa
wakizitaka wao” alisema.
No comments:
Post a Comment
https://www.facebook.com/gomesamohamedi