Tuesday, December 25, 2012

Super Nyamwela ahamia Bongo Fleva

MNENGUAJI wa kundi la Extra Bongo, Hassan Nyamwela ‘Super Nyamwela’ amekamilisha video ya wimbo wake mpya wa Maneno, akimshirikisha Amini Mwinyimkuu ‘Amini’.
Nyamwela alisema  ameamua kubadilika kimuziki kutoka katika uimbaji wa muziki wa dansi mpaka bongo fleva.
Alisema yeye ni mwanamuziki hivyo kubalika kwake hakumuathiri kitu chochote huku akiamini anaweza kufanya vizuri zaidi ya mwanzo.
“Mimi ni mwanamuziki na naweza kuimba chochote katika muziki” alisema.
Super Nyamwela alisema katika bendi ya Extra Bongo yupo kwa mkataba, hivyo haumzuii kufanya kazi yoyote ya muziki.


No comments:

Post a Comment

https://www.facebook.com/gomesamohamedi