Monday, July 16, 2012

Mwanza yachachamaa EBSS 2012

usaili wa Epiq Bongo Star Search unaoendelea Mwanza katika uwanja wa CCM Kirumba. Ikiletwa kwenu kwa ushirikiano wa kampuni yako ya hapa hapa Tanzania –Zantel. Mwamko wa washiriki umekuwa mzuri kuzidi mikoa mingine yote tuliopita msimu huu. Kwani mpaka mwisho wa siku jana jumla ya washiriki 480 walikuwa tayari wameshasajiliwa na bado usaili unaendelea siku ya leo. Pia katika eneo la usaili tuko na watu wa damu salama wakihamasisha watu kuchangia damu na mwamko wa washiriki umekuwa mzuri. Majaji wameshafika eneo la usaili na usaili umeshaanza. Pamoja na usaili, Zantel ilipata nafasi ya kukutana na madiwani wa mkoa wa Mwanza na kuwagawa jumla ya simu za mkononi 50 zilizounganishwa na mtandao wa Zantel chini ya kifurushi cha CUG (Closed User Group) ambao utawawezesha kuongea bure kati yao.
Mawazo na michango yenu yanahitajika katika kuendeleza uhusiano mzuri na katika kupata taarifa/picha bora zaidi. Kama utapenda tuongeze anuani ya barua pepe ili kupata taarifa zitakazo kuwa zinatumwa, tafadhali ongeza anuani hiyo na ujibu barua pepe hii ukiweka majina na wadau wengine wa habari.



Madam Rita akihojiwa na mwandishi kutoka Barmedas.

No comments:

Post a Comment

https://www.facebook.com/gomesamohamedi