| Wakati wasanii mbalimbali ambao wanaunda kundi la muziki maarufu kama Bongo Fleva na wale wa filamu wanaojulikana sana kwa jina la Bongo Movie wakijiandaa na mpambano mkali katika Uwanja wa Taifa wa mpira uliopo Dar es salaam, siku ya Saba saba katikaTamasha la Tumaini, hali imeshaanza kuwatisha baadhi ya wasanii katikamakundi yao. Wapo ambao wamepoteza tumaini kwakuwa hawawaoni wasanii wenzao ambao wamekuwa wakiwategemea katika michezo yao, na wapo ambao wanasikia wasanii wenzao siku hiyo watakuwa na show sehemu mbalimbali hao ni katiya wale wa Bongo Fleva, lakini Bongo Movie wanatamani kuwaona wasanii wa Bongo Fleva wote wakiwemo na kuwatia aibu kama wao walivyotiwa aibu kwa kupigwa 2-0 katika kuchangia waathirika wa Mabomu wa Gongolamboto. Kilammoja na hamu yake, ila wengine hofu ya kutoneshwa vidonda kwa kupigwa magoli mengine na kuyarudia matokeo ya mwanzo |
No comments:
Post a Comment
https://www.facebook.com/gomesamohamedi