Zantel yazidi kuinogesha EBSS Arusha, yatoa simu kwa madiwani wake, vijana wengi wajitokeza katika usaili
Katika usaili uliofanyika,zaidi ya washiriki 750 walikutana na majaji
na watu wasiopungua 1800 walijitokeza eneo la usaili. Majaji waliweza
kutoa maoni yao juu ya vipaji vilivyojitokeza na kuhakikisha
waliochaguliwa watakwenda kuwakilisha vyema mkoa wa Arusha. Katika matukio ya kijamii, Zantel imetoa
simu za mkononi 25 kwa manispaa ya jiji la Arusha ili kuwarahisishia
mawasiliano viongozi na watumishi wa manispaa.Simu hizo ambazo
zitasambazwa kwa Msitahiki Meya, Madiwani na mkurugenzi wa mji,
zitawarusu kupiga simu bure wakati wote kwa kutumia huduma ya kipekee ya
Zantel ya ‘CLOSED USER GROUP’.Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo,
Mkurugenzi wa masoko wa Zantel, Bwana Deepak Gupta, alisema kampuni yake
ina mkakati madhubuti wa kushirikiana na serikali ya Tanzania katika
kusukuma gurudumu la maendeleo. ‘Kwa simu hizi ambazo zina laini ya
Zantel, watumishi wa manispaa wanaweza kuwasiliana bure kabisa baina yao
hivyo kurahisisha mawasiliano na ushirikiano kwa vitengo mbambali vya
manispaa pamoja na kupunguza gharama’ alisisitiza Bwana Gupta.
Usaili unaendelea katika mikoa mingine ambapo wiki ijayo usaili utafanyika mkoani Mwanza tarehe 14 na 15 za mwezi huu wa Agosti Mawazo
na michango yenu yanahitajika katika kuendeleza uhusiano mzuri na
katika kupata taarifa/picha bora zaidi. Kama utapenda tuongeze anuani ya
barua pepe ili kupata taarifa zitakazo kuwa zinatumwa, tafadhali ongeza
anuani hiyo na ujibu barua pepe hii ukiweka majina na wadua wengine wa
habari.
Kijana huyu ni mmoja kati ya vijana wlaiojitokeza Arusha kushiriki katika usaili wa EBSS lakini hakupata nafasi hiyo
Huyu nae alivutia sana kwa kulipiga gitaa kiumakini lakini hata hivyo hakupata
Majaji walilazimika kusimama ili kuhakikisha kuwa wanapata vema alama za kila mshiriki wa EBSS Arusha
Mwana dada Amina S Maliam alionesha umahiri mkubwa wa kuimba siku ya kwanza lakini hata hivyo siku ya mwsiho hakuweza kufanya vema na alijikuta akiangau kilio sana
Alilazimika baadae kumfuata MadamRita kuomba ushauri wa kazi yake hiyo na aliahidiwa kusaidiwa
Amina hapa akiwa na mwanaye nani ya Club Triple A - Arusha kwenye usaili wa Epiq Bongo Star Search
No comments:
Post a Comment
https://www.facebook.com/gomesamohamedi