Sunday, April 15, 2012

Waliozitwaa tuzo za Kili

Shindano la Kilimanjaro Tanzania Music Awards 2012, jana limefikia ukingoni baada ya kutoa tuzo kwa wasanii ambao wamestahili kupata tuzo hizo kutokana na mashabiki wa muziki huo, kupiga kura kwa leo la kufanikisha nani anastahili kupata tuzo hiyo.
Katika tuzo za mwaka huu kumetawaliwa na majigambo, mafumbo, mitindo na vituko vya hapa na pale, ilimradi kuleta radha tofauti.
Lakini kwa kuanza tunataja kila msanii na tuzo yake aliyochukua,  1. Wimbo Bora Wa Reggae- Arusha Gold by Warriors from East (2) Wimbo Bora wa Dancehall- Maneno Maneno by Queen Darlin' (3) Wimbo Bora Zouk Rhumba- Dushelele By Ally Kiba (4) Wimbo bora wenye vionjo vya asili- Vifuu Tundu By A.T (5)  Wimbo Bora wa Taarab- Nani kama Mama By Isha Mashauzi (6) Wimbo Bora wa Kiswahili(Bendi)- Dunia Daraja By Twanga Pepeta(7)Wimbo Bora wa Afro Pop- Hakunaga By Suma Lee (8) Wimbo Bora wa R&B- My Number 1 Fan By Ben Pol
(9) Wimbo Bora wa Hip Hop- Mathematics By Roma (10) Msanii Bora Anayechipukia- Ommy Dimpoz (11) Rapa Bora wa Bendi- Kitokololo (12) Msanii Bora wa Hip Hop- ROMA (13) Wimbo Bora wa Kushirikiana- Nai Nai By Ommy dimpoz ft Ally Kiba (14) Wimbo Bora Afrika Mashariki- Kigeugeu By Jaguar (15) Mtumbuizaji Bora wa kike- Khadija Koppa 16. Mtumbuizaji Bora wa Kiume- Diamond Platnumz (17)

Mtunzi Bora wa Mwaka- Diamond 18. Producer Bora Wa Mwaka- Maneck (19) Video Bora ya Muziki ya mwaka- Moyo Wangu By Diamond (20) Wimbo Bora wa mwaka- Hakunaga by Suma Lee

 (21) Hall Of Fame(Taasisi)- JkT Taarab -Hall of Fame(Binafsi)-King Kiki -Hall of Fame(Binafsi)- Remmy Ongalla (22) Mwimbaji Bora wa Kike- Lady Jay Dee (23) Mwimbaji Bora wa Kiume- Barnaba



 Bonyeza hapo chini kidogo 'Read More'  kupata picha zaidi.... Endelea kuwa na BONGO UNIT siku zote