Tuesday, April 3, 2012

Nichumu- Yawa msumali kwa Lulu na Bob Junior

Nyimbo mpya ya Bob Junior imezua jambo baada ya mwanamuziki huyo kuandikwa kwenye gazeti moja la usukununu aka Udaku na udakuzi kwamba wapo kwenye In relationship  na mwanadada wa Bongo Movie Lulu. Ukweli ambao umechimbuliwa na Bongo Unit  kwa asilimia kadhaa mwanamuziki huyo na mwigizaji umegundua ni kweli hasa baada ya Bob Junior kuojiwa na hatmaye kukosa la kusema.

Bob Junior anasema kwamba ni kweli anakuwa naye pamoja tena kwa karibu  lakini ni kirafiki jambo ambalo lilipelekea kuja pamoja katika wimbo wa Nichum.

Hata hivyo Bob Junior amesema yapo mengi zaidi ataongea kuhusu na hisia hizo za watu, lakini kwa muda huu bado yupo njia panda kwakuwa wamemkaba koo kuhusiana na ishu hiyo.

Anasema anamengi ya kuongelea kuhusu Video yake ya Nichumu, ambayo ilianza kuzua gunzo hata kabla ya kushoot kwake, na kuhusishwa na matukio mbalimbali, ikiwemomoja la kutetea ndoa ya jinsia moja 'Ushoga na Usagaji'