Friday, April 27, 2012

Exclusive; Cloud 112 augua ghafla

Msanii maarufu wa filamu nchini Issa Mussa 'Cloud 112' amelazwa katika hospitali ya Al Ijumaa iliyopo Kariakoo baada ya kuugua ghafra, wakati akiwa katika shughuli zake za kawaida.  Cloud 112 amelazwa hospitalini hapo tangu saa saba mchana,na hivi sasa tayari ameshapata vipimo vya Malaria ambayo amekutwa hana, pia akapimwa na presha ambapo alikutwa ipo sawa, hali iliyopelekea kuchukua vipimo vya typhod. Hadi hivi sasa msanii huyo bado yupo hospitali kwaajili ya kuendelea kuangalia afya yake na kuchukuliwa vipimo zaidi, wakati huo pumzi ndiyo inayomsumbua kwa kuwa anaipata kwa tabu.
Cloud112 akiwa amelala pamoja na dripu ya maji