Thursday, March 15, 2012

Bob Junior atoa burudani kwa watoto wenye ulemavu

Mwanamuziki ambaye umaarufu wake kila siku unazidi kuwa mkubwa, Bob Junior 'Rais wa Masharobaro' wote waliopo duniani pia anajulikana kama Mr Chocorate, pia hutokosea kama ukimwita pia Shombeshombe, ila kwa sasa ameongezeka cheo kingine baada ya kutembelea shule ya walemavu iliyopo Kurasini Shimola Udongo inayoitwa shule ya msingi Jeshi la Wokovu. Cheo hicho kilikuja pale msanii huyo alipoamuakuwatembelea watoto hao na kuwa msanii wa kwanza kufika hapo
Bob Junior hakuwa hiyana nao,aliwaonyesha swaga zake kwa kuwapigia show kali, pia akawapamisaa mbalimbali, ndipo watoto hao walipovutiwa naye na kumpa jina la Rais wa Jeshila Wokovu katika shule hiyo.

Watoto pia walimuomba msanii huyo awe anawakumbuka mara kwa mara, na pia aliwaomba wawe anawapelekea vifaa vya muziki jambo ambalo Bob Junior alikubaliana nao na kusema atawapelekea

Bob Junior pia amewataka wasanii wenzake kuiga mfano huo wa kuwajali watu wenye ulemavu kwani wao pia ni watu na ndiyo mashabiki namba moja wa muziki wa Bongo Fleva.

No comments:

Post a Comment

https://www.facebook.com/gomesamohamedi