Mwanamuziki kutoka kundi la Sharobaro Rec, Raheema Rummy ‘Bob
Junior’ amesema hadi sasa bado yupo njia panda juu ya video moja kati ya video zake
tatu ya Ngombe, Singasinga na Nichumu.
Akizungumza na mwandishi wa safuu hii amesema kwamba wimbo
wake wa Singa singa ameufanyia Ulaya, na zingine amezifanyia hapa lakini zote
alihitaji zitoke kipindi hiki.
Amsema hali hiyo imemfanya aangalie sana upepo wa muziki kwa
sasa ili ajue huenda anaweza hata kuziachia zote kwa wakati mmoja.
|