Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe.
Khamis Hamza Khamis ameelekeza kiwanda cha nguo cha A to Z kilichpomkoani
Arusha kikamilishe ujenzi wa mtambo wa kutibu maji taka ndani ya miezi miwili.
Ametoa maelekezo hayo jana alipofanya ziara ya
kukagua nakufuatilia utekelezaji wa maagizo ya Serikali kuhusu kuondoa changamoto
ya harufu na maji taka ya nayotirirka kupita mtaro unaopita kwenye makazi ya watu.
Pia, ameelekeza Baraza
la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Kanda yaKaskazini,
wataalamu wa mazingira kutoka Ofisi za Mkuu wa Mkoa, Wilayana Halmashauri ya jiji
la Arusha kufanya kazi kwapamoja kuhakikisha maeleekezo hayo yanatekelezwa.
“Hamuwezi kujua hizi harufu
mbaya za haya maji taka yanayotoka hapana kutiririka kwenye makazi ya watu zinaathari
gani, sasaninatoamiezimiwilimkamilishemtambowahuu,” alisema Mhe. Khamis.
Aidha, naibu waziri huyo
alisema kiwanda hicho kimekuwa kikilamikiwa na wanachi kwa muda mrefu kwa uchafuzi
wa mazingira kwakutiririsha maji taka katika makazi ya wananchi.
Hivyo, kutoka na nahali
hiyo Serikali imekuwa ikichukua hatua mbalimbali kwakutoa maeleekezo kwauongozi
wa kiwanda kujenga mtambo wakusafishia maji taka kabla ya kwenda kwenye mazingira.
No comments:
Post a Comment
https://www.facebook.com/gomesamohamedi