Wednesday, October 28, 2015

Omary Clayton aomba kupigiwa kura kuibeba Tanzania



MWIGIZAJI wa filamu nchini Omary Clayton amewataka Watanzania kuweza kujitokeza katika kumpigia kura mitandaoni ili kumuwezesha kushinda msanii bora katika tuzo za Califonia Viewers Choice kupitia filamu ya Dogo Masai.


Clayton alisema katika tuzo hizo ambazo zinafanyika nchini, Marekani anawania pamoja na wasanii wengine kutoka katika mataifa makubwa, lakini tumaini lake limebakikwa Watanzania.

Aliwataja wanaowania pamoja katika nafasi ya msanii bora, yupo  Erick Calderon filamu  Insomnia kutoka Costa Rica , Daria Merlin filamu 9 Waves kutoka Spain, Seppe Cosyns filamu ya Fear  kutoka Belgium  Veron aldershoff filamu Justice is mind kutoka Marekani.

Aliwataka wasanii na kila mtu ambaye anapambana kwaajili yakulitakia taifa heshima, kuweza kumuunga mkono na kumpigia kura.
ingia hatakumpigia kura.... http://covcawards.wix.com/covcawards#!dogo-masai-feature-film/xjvq3




No comments:

Post a Comment

https://www.facebook.com/gomesamohamedi