Wednesday, July 18, 2012

Watu 60 watangazwa kufa kwenye Mv Seagul

Taarifa kutoka kwenye meli Seagul ambayo inasadikiwa imebeba abiria  takriban 280 imezama katika Bahari ya Hindi  eneo la Chumbe kisiwani Zanzibar inasema kwamba watu takribani 60 wamekufa kwenye ajali hiyo.  Meli hiyo ambayo inatumia  jina SKAGIT ilikuwa inatoka Dar Es Salam kuelekea Zanzibar,  kwa taarifa kutoka  kwa  vikosi vya wanamaji , inasema kwamba meli hiyo ilianza kupata matatizo baada ya kutokea mawimbi makali.  Hata hivyo Jeshi la polisi la wanamaji nchini Tanzania limeanza shughuli za kuwaokoa watu zaidi ya mbia mbili wanaohofiwa kuwa kwenye meli ya Skagit inayoripotiwa kuzama huko visiwani Zanzibar.
Kwa mujibu wa taarifa za polisi, ingawa hawajathibitisha idadi kamili ya abiria waliomo kwenye meli hiyo, lakini wamethibitisha kwamba meli hiyo imepigwa na dharuba ya upepo mkali katika eneo la Chumbe pindi ilipokuwa inatoka jijini Dar es Salaam kuelekea visiwani Zanzibar.
Itakumbukwa kwamba, ni takriban mwaka mmoja sasa tokea ajali ya meli iliyokuwa imezidisha mizigo kuzama katika pwani ya kisiwa cha Zanzibar ikiwa na watu takriban 800.

No comments:

Post a Comment

https://www.facebook.com/gomesamohamedi