Video zilizochukuliwa leo kwenye banda la Zantel Saba Saba ambapo
Majaji wa EBSS walipata nafasi ya kutembelea kujionea maonyesho
yanaondelea ikiwa ni pamoja na kukutana na waandishi wa habari kuelezea
waliyoshuhudia katika usaili wa mikoa mitatu waliyopitia ya Dodoma ,
Zanzibar na Lindi . Pia waliweza kutoa sifa wanazoziangalia katika
kutafuta vipaji vya muziki pamoja na kueleza eneo la usahili unaofuata
wiki hii plae mjini Arusha sehemu inayoitwa Triple A.
Pamoja
na hayo, Mkuu wa Masoko kutoka Zantel bwana . Deepak K. Gupta na Mkuu
wa mawasiliano Awaichi Mawalla walipata nafasi ya kuelezea njia mpya
ambayo wenye vipaji vya kuimba lakini wakakosa nafasi ya kufanya usaili
wanaweza kufanya usaili kupitia simu zao za mkononi. Mfumo huu ni wa
sauti ambapo mshiriki anapewa nafasi ya kuimba nyimbo aitakayo kwa muda
usiiozidi dakika moja na kuweza kupata nafasi ya kusikilizwa na Majaji.
|
No comments:
Post a Comment
https://www.facebook.com/gomesamohamedi