| Mwanamuziki nguli wa muziki wa kizazi kipya Judith Wambura jana Juni 15 alikuwa akisherekea siku ya kuzaliwa kwake, wakati huo Mc wa sherehe hiyo alikuwa Elias Barnaba 'Barnaba Boy au Barnaba Classic', ambaye pia aliungana na mwanamuziki huyo katika kutupa vipande vya nyimbo zake ikiwemo ile ya Njia panda ambayo iliamsha watu kwenye viti. Jide alifanya sherehe hiyo wakati mumewe Gadner G Habash hakuwepo, lakini hata hivyo sherehe ilienda vizuri ingawa watu wengi walitaka kujua nini kilijili, maana si kawaida na waliotegemea huenda likatolewa taarifa yoyote ya kutokuwepo kwake lakini jambo ambalo halikufanyika. Sherehe ya kuzaliwa kwake iliudhuliwa na wasanii mbali mbali ikiwemo wa muziki wa kizazi kipya watangazaji pamoja na wanamuziki wa taarabu. |
No comments:
Post a Comment
https://www.facebook.com/gomesamohamedi