Wednesday, May 23, 2012

Stive Nyerere kusaidia watoto yatima

NYOTA wa filamu nchini Steven Nyerere kesho saa 6 mchana anatarajia kutoa shukrani zake kwa watoto yatima na kusali misa fupi katika kanisa la Ananasifu katika kutimiza ahadi aliyoiweka katika uzinduzi wa filamu yake ya Mr Presedent.
Stive alisema kufanya hivyo ni kuonyesha shukrani zake kutokana na kwenda vizuri kwa filamu yake, na aliahidi kwamba lazima atoe japo sadaka kidogo kwa  watoto waishio mazingira magumu.
Alisema pia ameshaachia filamu yake mpya ya Respect Nyerere, ambayo anaamini nayo itafanya vizuri kama ilivyokuwa kwa Mr Presedent.
“Kazi zangu zitaendelea kuwa za kuhamasisha na kutoa mafunzo  zaidi na sio za mapenzi kama wengine wanavyofanya” alisema.

No comments:

Post a Comment

https://www.facebook.com/gomesamohamedi