| Filamu ya TOBA ya Cloud 112, inatarajiwa kuzinduliwa hivi karibuni kwa mtindo wa kipekee, kwa kumuarika kiongozi wa juu jambo ambalo halikuwahi kufanywa na mtu yoyote. Cloud 112, alisema katika uzinduzi wa filamu hiyo aliyoifanya katika kisiwa cha Kigamboni, anatarajia itazinduliwa na makamu wa kwanza wa raisi Zanzibar, Maalim Sefu Sharifu Hamad. Amesema filamu hiyo itazinduliwa rasmi saa tatu usiku katika hoteli ya Bwawani, lakini shughuli nzima itaanza saa moja usiku 18 may mwaka huu. |