Wednesday, April 25, 2012

Tmk na wasanii kibao kufunika Iringa

Meneja wa kundi la Tmk Wanaume Family Mkubwa Fella,  ameungana na wasanii zaidi ya kumi na mbili katika ‘Party’ maalum  ya burudani mkoani Iringa. Kiongozi wakundi hilo Saidi Fella  alisema kwamba Party hiyo  katika mkoa wa Iringa itafanyika May 6 katika kiwanja cha Samora, na baada ya kuombwa na mashabiki wa burudani wa mkoa huo baada ya kukaa kwa muda bila ya kufanya tamasha mkoani hapo.
Aliwatajabaadhi ya wasanii ambao watakuwepo kwenye rist hiyo ya kutumbuiza ni  Feroozi Mrisho’Ferooz’, Zuwena Mohamedi ‘Shilole’, Berry Black, Nurudini ‘Baba Kitorondo’, Saidi Juma, ‘Chege’, Amani Temba ‘Muheshimiwa Temba, Aslay Sadiq ‘Dogo’ Aslay, Ize Man, Dogo Muu na wengine.
(Dogo Aslay)
Pia alisema hata hivyo ijumaa ya may 4 wanatarajia kundi hilo lote kufanya tamasha mkoani Songea katika ukumbi wa jambo Lee wakati mchana watakuwa kwenye viwanja vya Majimaji.
Shilole
Bibi Cheka