Thursday, April 12, 2012

ROMA afunguka baada ya kumzika Kanumba

TULIJADILI HILI-TUMESHAMPUMZISHA NDUGU YETU KATIKA NYUMBA YAKE YA MILELE...MUNGU AMREHEMU!! But kuna mengi yamekuwa yakizungumzwa...
1. Kitendo cha mh. Rais kuhudhuria....msibani...pale nyumbani Sinza!!watu wanamlaumu mh.rais kwamba...wamefariki viongozi wengi wakubwa kama wakuu wa mikoa,wabunge,wakuu wa majeshi lakini hakuhudhuria akatuma mwakilishi, lakini kwa kanumba amekwenda!! Watu wanazidi kufunguka kuwa kwa kwenda kwa rais haoni kama ametumia nguvu kubwa ya ulinzi kumlinda pale pamoja na viongozi wengine, ambayo ni gharama kubwa!!why asingetuma mwakilishi tu! Je kanumba ni special kuliko mkuu wa mkoa au mbunge? pia ikalaumiwa pia eti kwanini serikali inapoteza pesa kupanga matrafiki,askari wengi ktk msiba huu, mwingine akasema gharama za mafuta ya ile helicopter au zile mil kumi za J.K aliyotoa km rambirambi eti angezipeleka tu kwa watoto yatima!! sio yakasemwa mengi sana! lakini  mie naamini rais hajafanya kosa...ktk marais wote wa Tz waliopita ikumbukwe huyu ndo' rais aliye karibu sana na sanaa, na ana mapenzi na wasanii, so amefanya yale kwa upendo  mkubwa...kwasababu kanumba alitangaza bendera yetu nje ya nchi pengine hata pasipo suport ya serikali!! So kwa hili mimi simlaumu mh.rais...ww unaonaje?
2. Lakini jingine ni kuhusu APPRECIATION...nimekuwa nikiliongelea sana hili, kuwa wabongo hatuna kawaida ya kukubaliana sisi kwa sisi...marehemu kanumba mara kwa mara tulikuwa tunakutana nae, maisha club,Leaders club,coco beach, kwenye live band,maofisini,hata barabarani, lakini  tulikuwa tukimpotezea tu pengine hata salamu hatukuwa tunampa....hata movie zake wengine walidiriki kuziponda, aah hawezi huyo movie itakuwa bongo?movie ni 24 na prison break bn! Wengi hatukuwa watu wa kumpa mawazo chanya bali kumponda na kumdiscourage!! lakini  jamaa hakukata tamaa alikuwa anajua anachofanya!! ...so enzi za uhai wake...wengi sio wote hatukuwa watu wa kumkubali kama inavyoonekana hapa!! Najiweka miongoni mwao ili kuleta attention ya hiki ninachoandka!! lakini  tazama leo alipofariki ule umati wote unalia,unaomboleza kwa majonzi, unaonyesha wote wanamkubali WHY?